lirikcinta.com
a b c d e f g h i j k l m n o p q r s t u v w x y z 0 1 2 3 4 5 6 7 8 9 #

lirik lagu njoo uichukue – mrisho mpoto

Loading...

eeeh eeh
roho yangu kama itakusaidia (ndugu yangu) kama itakupa ushindi
moyo wako najua
kama itakusaidia kama itakupa ushindi moyo wako najua
usiku rafikibwa giza
basi njoo uichukue×3
uichukue
basi njoo uichukue×3
ama kweli kama hujui unapo kwenda huwez kupotea na watu kukimbia wanakozika hudondokea kwenye mait nyama.

siku zote naamin mtu huwez kulala kwenye mto hata kama umekauka
na ukitaka kujua mwendo wa mjinga mpe kilemba uone

hili niombi langu toka kw-ngu kuja kwako

kama ya kw-ngu itakusaidia chochote kwenye ushindi wako niko tayari kukupa ila uifuate nyumban wala sio mbali!

nakuk-mbusha ukitaka n’zi wasikufuate achakula vilivyooza chuki humchoma aliyeihifadhi kwenye moyo tu siku zote
nakuuliza unatak kuja mchana ama jioni maana kila njia na muda wake najua mara nyingi ungependa kuja mchana ili uenekane
naomba nikuelekeze hivi pita uwanja wa taka hadi mfereji mchafu
kisha kibanda cha mbavu za mbwa katiza usisikie na mtu njiani endelea kuja
ni kioo tu pekee yake ndo huonyesha doa la kwel kwenye paji la uso
katiza choo cha gunia pembeni maskani camp taliban camp
ukisikia harufu kali bana pua haraka hapo choo kinapakuliwa na kutia moyo tu njoo karibia unakaribia kufika

kama itakusaidia (itakusaidia) kama itakupa ushindi(moyo wako najua)×2
usiku rafiki wa giza
uliza baba ubaya aliyetoroka jela au mama mwantum anayesutwa kila kukicha
ukiogopa kupotea uliza babu nshuba kikongwe muuza bangi atakupa uchochoro utapita ubavu ubavu
kila hatua utakayopiga k-mbuka maji ya dafu hayanywei kwenye gl-ss na siku hizi kinachopandwa kwenye changarawe kinakua haraka kuliko kwenye udongo
nakuomba ukisikia kuntumtututu ujue kuna mtu anachezwa endelea kuja na ukisikia cherekooo watu wanasasambua endelea unakaribia
alama kubwa utakazokutana nazo ni visheti na chips dume, kashata na maandazi, chapati na uroge wa ubuyu, pweza na vijit vyake
ukiona sufuria la supu unakaribia maana nchi yenu nchi yetu pia hapa watu pale kinyesi na kondom ndo kwetu dampo dogo pale pembeni maji ya mtungi nyumbani huko
chumba cha baba hapa choo cha pipa pembeni
unakaribia
usiponikuta jua ya kwamba nipo ferry kuungaunga mwana kwenye samaki anayechafua anasafisha kwa kutupa hana hapo sasa umefika
vipi bado unaitaka na ya kw-ngu ikuongezee ushindi kama ndio kuna masharti mawili tu
pitia kwa yule mama kamuombe samahani na uumpe pole kwasababu kwa kauli zako alipoteza kitanda chake
na kwenye hela mkiweka picha zenu wekeni na za kwetu wakati mnatumia mtutumia na sisi
mwisho lakini sio kwa umuhimu kwenye kiapo chako cha kweli ongeza na majina yetu
basi njoo uichukue
basi njoo uichukue
basi njoo uichukue(roho yangu)uichukue
basi njoo uichukue
basi njoo uichukue
basi njoooo uichukue(roho yangu)
basi njoo uichukue uichukue
basi njoooooooooooooooo

lirik lagu lainnya :

YANG LAGI NGE-TRENDS...

Loading...