lirik lagu a confession of a mad philosopher – dizasta vina
maana ya uhuru huisha baada ya utambuzi
baada ya kutambua kwamba uhuru si maamuzi
maana kifungo na mipaka vinafanana
aliyekuambia kuna uhuru utaupata kakudanganya
ipo asili inayofanya mwili wako mashine
kufanya ugonjwa uwe jela alafu afya ni jela nyingine
mjamaa amemwaga damu tayari
awe huru ili akawe mtumwa kwa mabepari
chagua kufa ukiona waja hawalipi wema
kufa wokovu kilichokufa hakifi tena
kufa ni uhuru kamili tabu ni nini
haupo huru sasa uhuru wa kweli ni kaburini
unak*mbatia uhuru wa kuambiwa
wakati unaishi na haukuchagua kuzaliwa
uhuru hautafutwi msafiri pumzika kubali chai
hauwezi kuwa huru ungali hai
uhuru si halisi jamaa badili umbo
uhuru sio jibu hata usikariri fumbo
uhuru ni falsafa ya vitabu iliandikwa na mababu
tutaisoma na mwisho itabaki huko
anayehitaji uhuru aelewe
kuogopa kufa ni utumwa kwa maana kufa ndio uhuru wenyewe
hata uwe mfalme ambaye anatoa idhini
huwei kuwa huru uhuru wa kweli ni kaburini
freedom freedom
freedom freedom
freedom freedom
freedom freedom
ukik*mbatia mw*nga jua utaificha nuru
uhuru si kwa mwafrika k*mkimbiza mkabulu
kuutaka uhuru sana jamaa si dalili njema
kama upo hai na unahisi uko huru fikiri tena
cheo huleta nuru pahala nuru haifiki
na pesa ndio njia ya uhuru ukiimiliki
pesa na cheo upita kule hakuingiliki
alisema mlevi mmoja ambaye pombe tu imemdhibiti
mwathirika ambaye dawa za kulevya zimefunga
na anahisi yuko huru mara baada tu ya kuvuta
labda si kweli haupo huru ukijiongeza
maana ukishaujua uhuru tayari ushaupoteza
je utaniona chizi au mwivi
au pumbavu au mshenzi ninayeongea vituko
au utaamua ukae chini utafakari
kisha ukakubali ndoa ajira navyo pia vifungo
aliye huru ni nani nieleze mtoto anayeenda kwa viboko
au mlokole mtenda mema baada ya kutishiwa moto
au msomi elimu mpaka chuo kihakiki
i swera kama uhuru ndio huo siuafiki
anayehisi yuko huru pita mbele
piga kelele maana hata mungu wako hayuko huru
hawezi kubadili mipango hawezi k*muumba
mungu mwingine mkubwa kupita yeye
unaetafuta uhuru wa kweli utateseka
utapoteza damu utatoa machozi na utakesha
hauwezi kuupata maana hakuna ulipouweka
uhuru haupatikani kwa fedha
uhuru is priceless kwakuwa si bidhaa halisi
wenye chapaa walihakiki
utaniangusha sana ukishindwa kuamini
upo uhuru ila uhuru wa kweli ni kaburini
you’ve got no freedom
you’ve got no freedom
you’ve got no freedom
you’ve got no freedom
freedom freedom
freedom freedom
freedom freedom
freedom freedom
lirik lagu lainnya :
- kumpulan lirik lagu arkadia feat peter lanzani › lirik lagu hipersomnia – arkadia feat. peter lanzani
- kumpulan lirik lagu denay › lirik lagu non chiamarmi eroe – denay
- kumpulan lirik lagu hanibal › lirik lagu 72h – hanibal
- kumpulan lirik lagu brayton bowman › lirik lagu puff puff pass remix – brayton bowman
- kumpulan lirik lagu doriko › lirik lagu ロミオとシンデレラ -miku expo 2014 in indonesia live- – doriko
- kumpulan lirik lagu deine ludder › lirik lagu ein feste burg ist unser gott – deine ludder
- kumpulan lirik lagu reach the shore › lirik lagu cambiares – reach the shore
- kumpulan lirik lagu samuel seo feat 넉살 › lirik lagu ego expand (100%) – samuel seo feat. 넉살
- kumpulan lirik lagu t rich › lirik lagu withdrawal. – t.rich
- kumpulan lirik lagu yayvo › lirik lagu california summer – yayvo